Bondia mstaafu, Floyd Mayweather anatarajiwa kurejea ulingoni mnamo Mei 14, 2022 kupigana na Don Moore katika Pambano la raundi nane la maonyesho litakalofanyika Dubai.
Mayweather, 45 atapigana na mpinzani huyo ambaye alishinda mapambano ya kulipwa 18 kati ya 19 aliyocheza alipokuwa akipigana.
Mara ya mwisho Moore kupanda ulingoni ilikuwa mwaka 2018 wakati Floyd alistaafu rasmi mwaka 2017, pambano lake la mwisho ikiwa ni dhidi ya Conor McGregor.
Mara ya mwisho kwa Mayweather kuwa ulingoni ni mwezi June katika pambano la maonyesho pia liliokuwa la raundi 8 dhidi ya staa wa Youtube, Logan Paul.
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.