Kocha mkuu wa AC Roma Jose Mourinho amevikeji vilabu vinavyofuzu kwa hatua ya mtoano ya Ligi ya Europa kupitia mlango wa nyuma kama ‘papa walioshindwa Ligi ya Mabingwa’.

Kikosi cha Mourinho kiko kwenye vita ya kutinga hatua ya mtoano kupitia Kundi C baada ya sare ya 1-1 dhidi ya Real Betis na kuwaacha wakiwa nafasi ya tatu kwa pointi nne, nyuma ya Wahispania hao (10) na Ludogorets (saba). Roma bado watakuwa na matumaini ya kuifanyia mabadiliko Ludogorets na kusonga mbele kwa michezo miwili ya kucheza kundi hilo.
Sare hiyo, hata hivyo, ilimaanisha kuwa Betis walikuwa na uhakika wa kufika hatua inayofuata na kocha huyo aliulizwa ikiwa walikuwa wanapendelea Ligi ya Europa, na hivyo kumpelekea kuzifunga timu kama Barcelona na Juventus.
“Ninawaona Betis kama wagombea, lakini papa waliofeli wa Ligi ya Mabingwa watawasili, na watakuja kwa bidii,” Mourinho alisema, akizungumzia timu zinazoshuka kwenye Ligi ya Europa baada ya kumaliza nafasi ya tatu katika makundi yao ya Ligi ya Mabingwa.

Kocha huyo amesema kuwa hawafai kuja lakini ndio ukweli itakuwa ya kufurahisha, kufeli kwa ligi ya mabingwa. Miongoni mwa klabu ambazo kwasasa zimeshika nafasi ya tatu katika makundi ya Ligi ya Mabingwa ni Barcelona, Juventus, Ajax, Atletico Madrid na AC Milan.
Mourinho ambae ni Mreno aliongeza kwa kusema kuwa wanataka kupita na kumaliza nafasi ya pili, lakini wakimaliza wa tatu watakuwa wagombea wa kwenda kushiriki Ligi ya Konferensi.

Mechi ya Wikendi Roma anacheza dhidi ya Sampdoria ugenini.

