Rasmi Gattuso Kocha Mpya Valencia.

Mchezaji wa zamani wa AC Milan na Italia, Gennaro Gattuso, 44 rasmi ametangazwa kama kocha mpya wa Valencia licha ya awali mashabiki kupinga maamuzi hayo.

Mtaliano huyo ambaye amevifundisha vilabu vya Napoli na AC Milan inakuwa ni mara yake ya kwanza kufundisha nje ya nchi yake na amesaini mkataba wa miaka miwili mpaka mwaka 2024.

 

 

Kiungo huyo wa zamani wa Italia anajiunga na Valencia kuchukua nafasi ya Jose Bordalas ambaye aliachana na klabu hiyo mapema mwezi huu baada ya msimu kukamilika.

Gattuso hakuwa na timu tangu Mei 2021 alipoondoka Napoli baada ya kuiongoza kushinda taji la Coppa Italia. Mwaka 2021 alitajwa kupewa nafasi ya kuifundisha klabu ya Fiorentina lakini mkataba ulivunjwa kabla ya kuanza kuinoa timu hiyo.

 


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.