Watford wamemteua Vladimir Ivic, 43, mikoba yao ya ukocha kwa mkataba wa mwaka mmoja. Kandarasi hiyo itarefushwa kutegemea matokeo yatakayosajiliwa na kikosi hicho cha Ligi ya Daraja la Kwanza (Championship) chini yake.
Ivic ambaye ni kocha wa zamani wa Maccabi Tel Aviv ya Israel anamrithi mkufunzi Nigel Pearson aliyetimuliwa na Watford zikiwa zimesalia mechi mbili pekee kwa kampeni za msimu huu wa 2019-20 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kukamilika rasmi.

Licha ya Pearson kupigwa kalamu wakati ambapo Watford walikuwa wakipigania nafasi finyu ya kusalia EPL, kikosi hicho kiliteremshwa ngazi baada ya kupoteza mechi zote mbili chini ya kocha mshikiliz Hayden Mullins.
Kichapo cha 3-2 walichopokezwa na Arsenal katika siku ya mwisho ya msimu kilitamatisha kipindi cha miaka mitano ya Watford waliotinga fainali ya Kombe la FA mnamo 2019 kunogesha kipute cha EPL.
Ivic hana tajriba yoyote katika soka ya Uingereza ama akiwa mchezaji au kocha japo Watford wamesisitiza kwamba wameridhishwa na mbinu zake za ukufunzi.
“Ni mara yangu ya kwanza nchini Uingereza na itanilazimu kuzoea mazingira haya mapya haraka iwezekanavyo kisha nijitahidi kurejesha Watford kwenye EPL,” akasema Ivic aliyewahi kuvalia jezi za timu ya taifa ya Serbia katika siku zake za uchezaji.

Ujio wake ugani Vicarage Road kunamfanya kocha wa nne wa Watford katika kipindi cha miezi 12 baada ya kutimuliwa kwa Javi Gracia na Quique Sanchez Flores mwanzoni mwa msimu huu. Kuondoka kwa wawili hao kulimpisha Pearson kuingia Watford mnamo Disemba 2019.
Ivic alisalia huru baada ya kuwaongoza Maccabi Tel Aviv kunyanyua mataji mawili ya Ligi Kuu ya Israel. Awali, alikuwa amedhibiti pia mikoba ya PAOK FC aliowanyanyulia ubingwa wa Greek Cup.
Ametua Watford pamoja na makocha watatu waliokuwa wasaidizi wake kambini mwa Maccabi Tel Aviv.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


Furahav
Pambana uipandishe daraja.
Issa
Vladmir ni safi ipaishe watford tunataka tuione epl tena
Lydia Emmanuel Magoti
Pongezi kwake Vladimir kutua Watford kawanyeshe Kaz mzee baba
felister
hongera Ivic nina imani utafanya vizuri watford
Gabriel
Nigel Pearson kwa upande wangu namuona kocha mzur sana sema n mistake ambayo imetokea ila sio mbaya kwa upande wa Vladimir ivic kuwa kocha maana nae pia yuko vzur sana ninamatumain nae sana atasaidia Watford
Ernest
Vladimir Ivic ajipange kuirudisha Watford kwenye hadhi yake
Magdalena
vladimir yupo vizuri sana katika ufundishaji soka
Sadick
Vladmir Ivic amepewa mkataba wa mwaka mmoja maana yake anatakiwa kuhakikisha kwamba Watford inarudi EPL vinginevyo hana chake#meridianbettz
Mwajumah
Yupo vizuri sana Vladimir katika ufundishaji soka#Meridianbettz
lombo
saf
Genia Sikaluzwe
Good
Shafii
Ni jambo zuri kwa wartfod mashabiki wanasubili mambo mazuri kutoka kwake.
Janeflora malisa
Nice
Povel
Kila la kheri
Hope mwaikuka
All ze best coach
Devotha
Pongezi kwake
Sabrina
Natumai utaitunza vyema na utaiweka watford katika nafasi nzuri
Dorophina
Vladimir anakibarua kizito kuipandisha daraja Watford
Johnmary joel
Ajipange vizuri ili timu isonge mbele#meridianbett
aisha
Ni jambo zuri vladimir kutua watfod imekua kama bahati kwa watfod tunataka tuone kazi yako
Zeiyana
Ni kocha mwenye uwezo wake tunategemea mabadiliko kamkubwa sana kuiyona Watford kwenye ushindani
Caroline
Sawa sawa
Ester jackson
Ni kocha mzuri na anatakiwa kufanya vena zaidi mana kupewa mkataba Wa mwaka mmoja ni kama kupimwa uwezo wako ajitahidi sana uwe wa mafanikio zaidi
Salma ngende
Kila la heri
Theonestina
Hongera yake
David Pere
Vladimir Ivic ajipange kuirudisha Watford kwenye hadhi yake
warda
Safi sana