Saka Aipatia Arsenal Pointi 3

Mchezaji wa Arsenal, Bukayo Saka amefurahia bao lake lililoipa Arsenal ushindi mgumu wa 1-0 ugenini dhidi ya Bodo/Glimt kwenye Ligi ya Uropa na kuendeleza mwanzo wao mzuri wa msimu huu.

 

Saka Aipatia Arsenal Pointi 3

Goli hilo lilifungwa dakika ya 24 na kuipa The Gunners pointi tatu muhimu huku ikiendelea kusalia kileleni kwa kundi A. Mchezaji huyo mwenye miaka 21 aliifungia goli hilo lakini kukiwa na presha kwenye mchezo huo kutokana na kuwa na mashambulizi mengi ya wapinzani wao.

“Ilikuwa ngumu sana, na tulijua hilo hapo awali,” Saka aliambia BT Sport. “Hakuna jinsi wanaweza kushinda mechi zao 14 zilizopita Ulaya hapa na tutakuja hapa na itakuwa rahisi.”

Bodo alipata nafasi nyingi za kusawazisha mchezo, huku Amahl Pellegrino akipoteza nafasi kadhaa nzuri huku Runar Espejord na Ola Solbakken pia wakikaribia kufunga. Lakini Saka hakuwa na huruma kidogo kwa mabingwa hao wa Norway baada ya mechi, akisimulia uzoefu wa awali wa kuwa mwisho wa matokeo yasiyo ya haki.

Saka Aipatia Arsenal Pointi 3

“Hii ni soka, usipofunga unaadhibiwa,” Saka aliongeza. “Tumekuwa na michezo kama hiyo na tumeacha mchezo tukiwa na hisia ngumu sana, lakini utajifunza haraka huu ni mpira wa miguu.

Arsenal wanarejea London wakiwa na pointi nyingine tatu, lakini Saka anataka wachezaji wenzake waongeze umakini wao kabla ya mechi ya Jumapili ya Ligi Kuu dhidi ya Leeds United, ambao bado hawajapoteza katika Elland Road msimu huu.

Mchezaji huyo alisema kuwa wanapaswa kuwa na furaha na pointi tatu na kuzingatia kama anavyosema siku zote kuzingatia kila mchezo ni muhimu kwasababu mchezo unakuja kila baada ya siku tatu na inazidi kuwa ngumu, kwahiyo lazima tuweke umakini wetu kama zamani na kujaribu kushinda kila mchezo.

Saka Aipatia Arsenal Pointi 3

Hakusita kuzungumza kuhusu malengo yake binafsi ambapo alisema kuwa ni kushinda, na ni jambo muhimu kwake na ana uumini mkubwa wa kucheza kwanza hivyo timu ikishinda, naondoka uwanjani nikiwa na furaha.

Acha ujumbe