Wolves Kumsajili Diego Costa

Klabu ya Wolveshampton Wonderers inatarajia kumsajili  Diego Costa ambaye ni mchezaji wa zamani wa Chelsea na Atletico  anayecheza kama mshambuliaji. Mchezaji huyo anatarajiwa kuwa Uingereza wiki hii kwaajili ya kukamilisha uhamisho wake akitokea Atletico Mineiro ya huko Brazil. Diego anasajiliwa na Wolves akiwa kama mchezaji huru ambapo mkataba wake utakuwa hadi June 2023

Inaripotiwa kuwa Wolves wapo kwenye mazungumzo ya kina kwaajili ya kumsajili mshambuliaji huyo huku kukiwa na makubaliano katika kanuni juu ya makataba wa mchezaji huyo. Mpango huo unategemeana na vipimo vya matibabu ambavyo tayari vimepangwa na klabu hiyo.

Diego Costa mwenye umri wa miaka 34  amepita vilabu mbalimbali ikiwemo Chelsea ya Uingereza  ambapo alicheza kwa mafanikio makubwa, Atletico Madrid ya Hispania Valladolid  na vilabu vingine vingi kabla hajatimkia huko Brazil.

Wolves Kumsajili Diego Costa

Wolves ambayo inaongozwa na kocha mkuu Bruno Lage hawajaanza msimu vizuri kwani ndani ya michezo sita ambayo amecheza ameshinda mchezo mmoja, sare tatu na amepoteza michezo miwili huku akiwa anashikilia nafasi ya 14 kwenye msimamo. Diego Costa atakuja kuongeza faida kwenye eneo la ushambuliaji kwani ni mchezaji mzoefu na anaijua ligi ya Uingereza.

Makala iliyopita

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.