Erik ten Hag amesema Antony atafanya mazoezi na wachezaji wenzake wapya kwa mara ya kwanza leo, baada ya kukamilisha uhamisho wake kwenda Manchester United siku ya Alhamisi.

Mbrazil huyo alikuwa mmoja wa wachezaji wawili walioongezwa siku za mwisho kwenye kikosi cha Mholanzi huyo, akijiunga pamoja na Martin Dubravka aliyesajiliwa kwa mkopo kutoka Newcastle United.

Antony alitazama mechi yao dhidi ya Leicester City akiwa nyumbani kwani mechi hiyo ilikuja mapema sana kwake, lakini Ten Hag hajapuuza uwezekano wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Arsenal katika uwanja wa Old Trafford Jumapili.

Kocha huyo amethibitisha kuwa winga huyo anatazamiwa kushiriki katika kikao cha timu Ijumaa alasiri huko Carrington, na kisha atafikiria kama mchezaji huyo wa zamani wa Ajax yuko tayari kujumuishwa kwenye kikosi.

“Kesho (Ijumaa), tuna kikao cha timu na Jumamosi tuna kikao cha timu, kwa hivyo nitafikiria kisha tutachukua uamuzi.”

Erik amekuwa na muendelezo mzuri wa kupata matokeo baada ya ushindi kwenye mechi 3 mfululizo huku mechi inayofuata huenda ikawa ni ngumu kwake kulingana na mpinzani wake anayekutana nae kuwa na mwanzo mzuri kwenye msimu kwa kushinda mechi zote 5 walizocheza.

