Mchezaji wa Al Ahly ya Misri Percy Tau alianzia benchi kwenye mchezo wa jana wa nusu fainali ya klabu bingwa wa dunia-FIFA dhidi ya Real Madrid na aliingia kipindi cha pili na kuonesha kiwango kizuri huku akimsumbua zaidi Camavinga. Odds kubwa za soka unazipata Meridianbet.

Al Ahly ilipoteza kwa mabao 4-1 na wababe hao wa Hispania huku Percy Tau alipopewa nafasi dakika ya 61 tu ya mchezo lakini akashindwa kufanya lolote.
Wakati huo huo, Kocha wa Real Carlo Ancelotti hakufurahishwa na kiwango cha timu yake katika ushindi wao akipendekeza walicheza chini ya kiwango katika mechi ambayo walipaswa kumaliza mapema. Ukiwa na meridianbet unaweza kubashiri mubashara, tembelea maduka ya meridianbet uweze kubashiri.
Baada ya Vinicius Jr na Federico Valverde kufunga kila mmoja wakati wa mapumziko, Real walipoteza nafasi kadhaa za kuongeza bao la kuongoza na Al Ahly wakapata pigo jingine baada kupigiwa penati iliyopanguliwa na Ali Maaloul.

“Tulipokuwa tukiongoza kwa mabao 2-0 (mapema kipindi cha pili), tulidhani kwamba mchezo umekwisha na tukaanza kupiga chenga nyingi mno,” Ancelotti aliambia mkutano wa wanahabari Jumatano.
“Hii ni michuano ambayo Real Madrid ina mengi ya kupoteza na hakuna cha kushinda,” Ancelotti alisema.
“Tulidhani kwamba mchezo ulishinda 2-0 na mambo hayako hivyo, tumepumzika na haiwezi kuwa hivyo.”
Real Madrid itamenyana na Al Hilal ya Saudi Arabia katika fainali mjini Rabat Jumamosi baada ya kuwachakaza mabingwa wa Amerika Kusini Flamengo ya nchini Brazil 3-2 katika nusu-fainali ya kwanza. Beti na Meridianbet mechi za ligi zote, odds ni kubwa sana, Usikose hii!!
Ancelotti alithibitisha kuwa mshambuliaji Karim Benzema na beki Eder Militao, ambao walibaki Madrid kwa ajili ya matibabu ya majeraha yao, watajiunga na timu siku ya Alhamisi na wanaweza kupatikana kwenye fainali. Pata Odds za soka ukiwa na Meridianbet.
“Wala hawajapona kabisa, Karim (Benzema) yuko vizuri lakini akiwa na Militao hayo ni mashaka zaidi.
“Ijumaa tutafanya maamuzi, (Dani) Carvajal alikosa mechi ya leo kutokana na homa na (Marco) Asensio kutokana na kuzidiwa kidogo, nadhani watakuwa tayari kwa Al Hilal.”

