MSIMU mwingine wa mchezo wa hisani wa Nifuate ambao upo chini ya Ali Kiba na Mbwana Samatta utafanyika Jumanne ijayo Azam Complex Chamazi na kwa msimu wa pili kutakuwa na mechi ya utangulizi ya wanawake ya Team Kiba na Team Samatta.
Msimu uliopita mechi hiyo ilichezwa kwenye uwanja wa Mkapa na matokeo kuwa suluhu. Mratibu wa mchezo huo Samatta Junior alisema: “Kuelekea msimu wa Nifuate 2023 tumepata bahati tena ya mchezo wa utangulizi kwa wanawake ambao utachezwa katika uwanja wa Azam Complex Chamazi siku ya tarehe 20 June 2023.
“Lengo kubwa ni kuhakikisha tunapata nafasi ya kuutangaza mpira wa miguu wa wanawake katika jamii yoyote ile, ili kuendelea kuuaminisha umma kuwa soka la wanawake ni sehemu ya ajira kwa watoto wa kike
“Siku ya SamaKiba kutakuwa na mashabiki wa aina mbalimbali kama mashabiki wa muziki na wale wa mpira hivyo italeta picha ya aina yake katika kuendelea kuutangaza mpira wetu.
“Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Jakaya Mrisho Kikwete.

