Xavi: Kuondoka kwa Dembele Kutatudhoofisha

Kocha wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez amesema kuondoka kwa winga wa kimataifa wa Ufaransa Klabuni hapo Ousmane Dembele kutawadhoofisha.

Xavi wakati akiongea na wanahabari kuzungumzia masulala mabalimbali ya klabu hiyo alisema anafurahishwa na mawinga waliopo ndani ya klabu hiyo, Lakini kuondoka kwa Dembele kuna namna kutacha pengo kwenye timu hiyo.XaviWinga Ousmane Dembele anatarajia kutimka klabuni hapo na kujiunga na mabingwa wa Ufaransa klabu ya PSG ambapo mpaka sasa wameshamalizana na yamebaki mambo machache kuweza kukamilisha dili hilo.

Kocha huyo na kiungo wa zamani wa klabu hiyo aliongeza pia kwa kusema alimuuliza Dembele ni sababu gani iliyomfanya akaichagua PSG mbele Barca na alichomjibu ni sababu binafsi ndio zimepelekea kutimka.XaviKocha Xavi amekua akimuhitaji Dembele aendelee kubaki ndani ya klabu hiyo na hata mara kadhaa alipokua akihojiwa alikua anaeleza wazi kua winga huyo wa kimataifa wa Ufaransa ni mchezaji muhimu ndani ya timu hiyo na angehitaji kua nae kikosini.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.