Baada ya kukamilisha usajili wa mastaa wapya kwa mafanikio makubwa, klabu ya Fountain Gate FC iko tayari kuonyesha makali mapya msimu huu. Oktoba 12, mashabiki watafurika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati, kushuhudia tamasha kabambe la kutambulisha kikosi kipya kilichosukwa kwa ustadi na malengo makubwa.
Katika hafla hiyo, afisa habari wa timu hiyo amesema kutakua na mchezo maalum wa kirafiki hivyo wakazi wote wa Babati pamoja na mashabiki wa Fountain Gate FC wajiandae kupata burudani kutoka kwa wachezaji hao.

Kikosi kipya kinatambulishwa zikiwa ni siku chache zimepita tangu FIFA watoe kibali cha kusajili kwa klabu hiyo ambayo awali ilikua imefungiwa kufanya usajili kutokana na limbikizo la madeni kutoka kwa wachezaji wao wa awali.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.


