Ligi kuu ya NBC Tanzania, iliendelea jana kwa michezo miwili ambapo mchezo wa mapema ulikuwa wa Yanga vs Dodoma Jiji ambapo vijana wa Pedro waliondoka na ushindi mnono kabisa wa mabao 3-1.

Mchezo huo ulipigwa katika dimba la KMC Complex ambapo nafasi kubwa ya kuondoka na ushindi alipewa Yanga kutoka na ubora wa kikosi alichonacho pamoja na kiwango ambacho anakionesha kwenye ligi kuu ya Tanzania hadi sasa.
Ushindi huo sasa unawafanya vijana wa mitaa ya Twiga na Jangwani kupanda hadi juu kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi zao 22 baada ya kucheza michezo 8 hadi kwenye kwenye ligi.
Mabao ya kuiteketeza Dodoma Jiji yalitupiwa kimyani na Depu, Abuya na Dube, huku kwa upande wa wageni bao lao la kufutia machoezi lilifungwa na Never Tigere na kuwafanya wabaki kwenye nafasi yao ya 10 kwenye ligi hadi sasa wakiwa na pointi zao 10.
Baada ya mchezo huo sasa mabingwa hawa wa Nchi wataigeukia mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF) ambapo watawakaribisha Al Ahly huku wakitaka kulipa kisasi baada ya kupoteza mechi yao ya mwisho kule Cairo. Je wanaweza kushinda mechi hii Yanga?


