Ligi kuu ya NBC Tanzania jana iliendelea kwa mchezo mmoja ambapo bingwa mtetezi Yanga alikuwa nyumbani kumenyana dhidi ya Mashujaa na akafanikiwa kushinda kwa mabao 6-0.

Mchezo huo ambao ulipigwa majira ya saa 10:00 katika dimba la KMC Complex ulimalizika kwa Wanachi kukusanya pointi 3 na uhsindi wa kishindo huku mashabiki wakifurahi kabisa kuona ubora wa klabu yao.
Mpaka kufikia mapumziko Yanga walikuwa wanaongoza kwa 3-0, huku wakiukamata mchezo kwa asiliia kubwa kabisa na burudani ambayo ilitolewa ilikuwa ni ya hali ya juu.
Mabao hayo ya kuimaliza Mashujaa FC yalifungwa na Damaro, Abuya, Pacome, Dube, Mudathir, pamoja na Depu ambaye ni usajili mpya wa Wananchi.
Kwa ushindi huo sasa Yanga wapo nafasi ya kwanza wakiwa na pointi zao 19 baada ya michezo 7 ambayo wamecheza hadi sasa, huku kwa upande wa Mashujaa wao wamesalia nafasi ya 5 wakiwa na pointi zao 13 hadi sasa.


