Kikosi cha Simba sc kimesafari kuelekea Singida kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa ligi kuu ya NBC dhidi ya Singida Black Stars utakaochezwa Machi 11, 2026 katika uwanja wa Airtel mkoani humo.

Timu hiyo imeondoka mapema leo kupitia uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam na kutua Dodoma mapema asubuhi, ambako itaweka kambi ya muda kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo muhimu wa ligi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa mujibu wa ratiba ya timu hiyo, kikosi cha Simba sc kitafanya mazoezi jioni ya leo jijini Dodoma kabla ya kuanza safari kuelekea Singida kesho mapema kwa ajili ya mchezo huo dhidi ya Singida Black Stars.


