Mshambuliaji wa Real Madrid fc Kylian Mbappé pamoja na kiungo mshambuliaji Jude Bellingham wamerejea kikosini baada ya kukaa nje kwa muda wakutibu majeraha yaliyokuwa yakiwasumbua. Kurejea kwa nyota hao kunatajwa kuwa nguvu kubwa kwa kikosi hicho kuelekea michezo muhimu ya mashindano ya Ulaya.
Mbali na Mbappé na Bellingham, beki wa kushoto wa timu hiyo Álvaro Carreras pia amerejea kwenye kikosi baada ya kupona majeraha ya hapa na pale yaliyomuweka nje kwa muda. Kocha wa Real Madrid fc ameamua kuwajumuisha wachezaji hao katika kikosi kinachoendelea na maandalizi ya mchezo ujao muhimu wa kimataifa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Timu hiyo sasa inajiandaa kusafiri kuelekea Manchester nchini United Kingdom kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa hatua ya mtoano dhidi ya Manchester City. Katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo, Real Madrid fc ilipata ushindi wa mabao 3-0, matokeo yanayowapa faida kubwa kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa katika dimba la Etihad.

