Usajili wa kwanza Baada ya Kurejea Zidane

Baada ya aliyekuwa meneja wa Real Madrid, Zinedine Zidane kurejea tena klabuni hapo, Real Madrid wanaripotiwa kuwa wamekubaliana kumsajili nyota mbrazili anayecheza nafasi ya ulinzi Eder Miltao kutoka Porto mwisho wa msimu huu.

Miltao ambaye ana umri wa miaka 21, alijiunga na Porto akitokea Sao Paulo mwaka 2018 na ameonekana kufanya poa kwenye Primeira Liga na Champions League.

Usajili wa kwanza Baada ya Kurejea Zidane
Eder Miltao

Makubaliano ya Real Madrid yanatajwa kufanikisha mkataba wa mika 6 na dau sharti la kumnunua la paundi milioni 50. Nyota huyu anatajwa kuwa na uwezo wa kucheza nafasi ya ulinzi upande wa kulia na pia ana uwezo wa kucheza kama kiungo pale inapohitajika.

Staa huyu atakuwa ni mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Real Madrid chini ya Zinedine Zidane kama meneja kwa mara yake ya pili klabuni hapo.

3 Komentara

    Sawa nakubali mwanetu

    Jibu

    Yuko vizuri kijana.

    Jibu

    Gud news

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.