Tshishimbi Aje Yoyote, Tuchuane

Kiungo wa DR Congo amekiri yupo tayari kupambana dhidi ya yoyote kuhakikisha anapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza.

Nahonda huyo wa Yanga SC, Pappy Tshishimbi amesema amejipanga tayari kushindana na yoyote katika nafasi yake kwenye kikosi.

Kumekuwa na taarifa kuwa Yanga inahusishwa na kiungo mkabaji wa Rwanda, Ally Niyonzima, na kama atasainiwa ataleta upinzani katika nafasi hiyo dhidi ya Tshishimbi.

Ally Niyonzima

Niyonzima inasadikiwa kuwa kwenye orodha ya wachezaji ambao kocha Luc Eymael ana wahitaji, na Tshishimbi amekiri yupo tayari kuchuana nae.

Tshishimbi amekuwa chaguo la kwanza kwenye kikosi cha wananchi pamoja na klabu kubadili makocha.

“Napenda ushindani, mara nyingi nashangaa watu kuogopa ushindani, lakini kwangu napenda kwasababu ushindani ndio njia pekee ya kuboresha kikosi.”

“Kukiwa na ushindani mkubwa kwenye timu, ndio wakati kikosi kinakuwa bora na bora zaidi. Kama Yanga watasajili kiungo mkabaji mwingine ni bora kwasababu ndio kitu natamani kuona.

“Anatakiwa atue mapema inavyowezekana, ili tuanze ushindani kwenye kwenye timu.”

4 Komentara

    Bora wanawajagwani waongeze majembe mengine

    Jibu

    Jagwani kitawaka🔥

    Jibu

    Ni kitu kizuri sana kujiamini

    Jibu

    Namkubaliii kinoma

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.