Kufuatia kuwa na msimu wenye maneno mengi kumuhusu kipa wa Manchester United – David De Gea, sasa ameamua kujikingia kifua na kuweka wazi lengo lake la kuipigania jezi namba 1.
Kwa misimu miwili iliyopita, De Gea anaonekana kushuka kiwango kwa kufanya makosa kadhaa ambayo yameigharimu timu kwa kiasi kikubwa. Inakumbukwa mechi ya nusu fainali ya Kombe la FA dhidi ya Chelsea, De Gea alifanya makosa mawili yaliyopekea kufungwa magoli mawili.

Wadau mbalimbali wa mchezo wa soka wamekuwa wakielezea hisia zao kuhusu kiwango cha De Gea,wengi wao wamekuwa wakimtaka Ole Gunnar Solskjaer kufanya maamuzi ya haraka na kumkabidhi mikoba kipa chipukizi Dean Henderson.
De Gea amenukuliwa akisema ” Ninajiamini, nimekuwa nikionesha ubora wangu kwa miaka mingi na hivyo muda wote ninapatikana kama kocha akinihitaji. Nipo tayari kucheza muda wowote na kuisaidia timu kama kawaida.”

Akizungumzia Mashindano ya Europa, De Gea amesema ” nadhani kiwango chetu kimeongezeka msimu huu. Tulikuwa tumezidiwa pointi 14 na timu iliyokuwa nafasi ya 3 kwenye Msimamo wa EPL lakini mwisho wa siku tumemaliza katika nafasi ya 3.
“Nadhani tumecheza vizuri kwenye michezo mingi. Kusema ukweli, tulistahili kucheza fainali. Pengine tulihitaji uzoefu zaidi kwenye kikosi na kutumia nafasi za kufunga tulizozipata. Tutaendelea kuongeza kiwango na kuipigania timu pamoja na kushinda mataji msimu ujao.”

Baada ya kumaliza msimu kwa kutolewa kwenye nusu fainali ya Michuano ya Europa. Wachezaji wa Manchester United wamepatiwa likizo ya wiki 2 kabla hawajarudi tena kwenye mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


magdalena
De gea wasimulaumu bure wamlaumu kocha aliepanga kikosi cha wachezaji wabovu de gea yeye kazi yake ni kudaka tu na si uchezaji
Ernest
Nasemaje maneno maneno yao Man U yatawaponza ngoja tuu De Gea apate deal sehemu nyingine
Zeiyana
Makosa yapo hakuna mtu hasiyekosea. De gea amefanya makubwa sana kwenye clabu ya man u kwa likizo waliyo mpa naamni kabisa kuna mabadiliko makubwa sana tutayaona kutoka kwake
rama
Maoni:bado kiwango chake kipo vizuri sana
Antony luseno
De gea bado united inamhitaji
Saupha mohamed
Huo ndo mchezo ago maneno katika game kitu chakwaaida tu..
Ester jackson
De gea yuko vizuri ingawa kuna mambo yanajitokeza lakini sio kwa kusudi naninaamini kuwa ni kila bora zaidi kama watamuacha Chelsea watamchukua tena
Tatu
De gea kwa msimu miwili iliyopita anaonekana kushuka kiwango kufanya makosa kazaa ktk timu ingawa ni mchezaji anayejituma sana
Nasra
Bado anahitaji kuongeza ujuzi
Dorophina
De gea yupo vizuri mbona na kiwango chake kipo vizuri
Caroline
Kwenye maisha kuna kupanda na kushuka
Sauda
Yupo kwenye kiwango kizuri sana
felister
mbona de gea ni kama anajihami hivi
Lydia Emmanuel Magoti
Msimlaumu De Gea usimamizi wakikosi kilikuwa sio poa nakwaujumla akuna kulaumiana nijambo lakulekebishwa
Shan
De gea ni kipa mzuri na wana man u wanatarajia kua atakua clubuni hapo msimu ujao.
Latifa juma mohamed
Ila bado yupo vizuri
Salma ngende
Ni vizuri anajiamin
Edgar
Ila timu nzima ya man u inazingua hususan upande wa forward.. muache degea ajikingie kifua
farida ahmadi
David de gea ni kipa mzuri Sana
Neema
Lazima ajikubaliii ila asijebwetekaa
Gabriel
De gea kiukwel msimu huu amezingua sana tuangalie Kama kwel ataweza kutetea jez namba 1 maana alipoangalia anapokonywa kabisa Henderson
Furahav
Ila bado yuko vizuri
Sabrina
De Gea yupo vizur ni mchezaji mwenye kiwango chake
Hope mwaikuka
Ni matokea tu ya mpira ila De Gea ni kipa mzuri tu
Fatuma kasomo
aongeze juhudi
Theonestina
Yuko vizur Sana
Shafii
Mi naamini de gea ni kipa bora Sana na katika soka kuna makosa madogo madogo ambayo yanatokea man u wakiruhusu kumuachia watakua wamepoteza jembe.
Povel
Maisha ya de gea ndani ya United naona yamefika ukingon
Sylvester
De Gea Inatosha Sasa tafuta timu nyingine tuachie Manchester yetu Dean Henderson arudi awe nambari moja
Janeflora malisa
Yupo vzr
Samiah
Yupo vzr
Mwajumah
Bado kiwango chake kipo vizuri sana # Meridianbettz
Fatina mfingi
Makal nzur
David Pere
Ila timu nzima ya man u inazingua hususan upande wa forward.. muache degea ajikingie kifua
Sadick
De Gea kutoka kuwa golikipa anayesifiwa hadi kujitetea , inawezekana ana tatizo jingine nje ya uwanja linaloathiri uwezo wake uwanjani#meridianbettz
Omary lukumbi
De gea ni goli kipa mzr sana ila kuna vitu kidogo vina hitaj marekebisho
Devotha
Kipa ninaemkubali sana
warda
De Gea bwana mie nisha mchoka