Guardiola - Muda Ukifika Nitasaini Mkataba.


Kocha Pep Guardiola, 49, amesema atatia saini mkataba mpya kambini mwa Manchester City iwapo atahisi “anastahiki” kufanya hivyo badala ya kupewa mkataba huo.

Kandarasi ya sasa kati ya mkufunzi huyo raia wa Uhispania na Man-City unatarajiwa kutamatika rasmi mwishoni mwa msimu huu na ni matamanio ya usimamizi wa miamba hao kumshuhudia Guardiola akirefusha muda wake pale Etihad.

Guardiola anaanza msimu wake wa tano kambini mwa Man-City mnamo Septemba 21 atakapowaongoza waajiri wake kuvaana na Wolves katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) katika uwanja wa Molineux.

 

Guardiola - Muda Ukifika Nitasaini Mkataba.

Hiki ndicho kipindi kirefu zaidi kwa Guardiola kuhudumu katika kikosi kimoja baada ya kudhibiti mikoba ya Barcelona (2008-12) na Bayern Munich (2013-16).

“Ningependa sana kusalia hapa Etihad kuwanoa Man-City. Nimeishia kuyapenda mazingira ya hapa ila nahitaji kustahili kupewa kandarasi mpya.

Man-City wamefaulu kujivunia mengi katika kipindi cha mwongo mmoja uliopita na ni lazima tuendeleze rekodi hiyo,” akasema Guardiola ambaye ni mchezaji wa zamani wa Barcelona.

Kwa mujibu wa Guardiola, hakuna yeyote kati ya Mwenyekiti Khaldoon Al Mubarak au Afisa Mkuu Mtendaji Ferran Soriano ambaye amewahi kumzungumzia kuhusu mkataba mpya.

Ingawa anahisi kwamba matarajio kutoka kwake ni ya kiwango cha juu hasa baada ya kusuasua kwao muhula uliopita ambao ulishuhudia tofauti ya alama 18 kati yao na mabingwa Liverpool.

 

Guardiola - Muda Ukifika Nitasaini Mkataba.

Man-City pia walibanduliwa na Olympique Lyon ya Ufaransa kwenye robo-fainali za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) na hilo likawapa Bayern kibarua rahisi cha kuifunga Lyon (3-0) kwenye nusu-fainali na hatimaye kutwaa ufalme baada ya kuwapiga Paris Saint-Germain (PSG) 1-0 kwenye fainali jijini Lisbon, Ureno.

“Wasimamizi wa Man-City hawakunipa masharti: kwamba lazima utimize haya au yale ndipo uongezewe mkataba. Waliniambia niongoze kikosi kucheza soka nzuri,” akatanguliza.

“Lakini najua hadhi ya klabu hii pamoja na matamanio yao. Matarajio kutoka kwa mashabiki pia ni ya kiwango cha juu. Lazima turejelee kushinda mataji,” akaongeza.


FURAHIA KASINO YA MTANDAONI

Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.

Cheza Sasa

38 Komentara

    Guadiola anahitaj atafute maisha mengine asiharibu cv yake kwa kufukuzwa

    Jibu

    Muda wako ukifika utasain tuu

    Jibu

    Uamuz ni wako

    Jibu

    Guadiola kama anahtaj kusepa na swala la champion league kama limekuwa kipengele sana hapo city pamoja na mabosi kumpatia fedha za kusajili wachezaj awatakao

    Jibu

    uamuzi anao yeye mwenyewe

    Jibu

    Namkubali sana Pep Giadiola

    Jibu

    Kweli guardiola haina maana kukufukuza muda ukifika itakua hivyo

    Jibu

    Mimi nadhani anataka fedha iongezeke

    Jibu

    Maamuzi anayo yeye

    Jibu

    Uwamuzi mzuri

    Jibu

    Pep no kocha Bora sana katika kipindi hiki, Nadhani kama mwenyewe pia atapenda kuwepo Mancity Mud mrefu nahisi hakuna kipingamizi

    Jibu

    guardiola aendelee tu kutulia apo city bado ana msaada mkubwa sana

    Jibu

    Mimi nadhani angetafuta chaka sehemu nyingine

    Jibu

    Guardiola ni bora asalie man city

    Jibu

    Yupo sahii Guardiola anacho kisema

    Jibu

    Maamuzi anayo mwenyewe

    Jibu

    Mbona Kama anasua sua kusaini huo mkataba

    Jibu

    Muda ukifika tutajua kama atasain

    Jibu

    Guadiola hana mengi ya kuifanyia man city kuondoka kwa sasa hitakua wakati mgumu clabuni pale

    Jibu

    Anapima upepo kwanza kuona mwelekeo wa timu kabla ya kusaini tena ama atafuta changamoto mpya#meridianbettz

    Jibu

    Kama ni heshima kashapata nchi mbali mbali kwa sasa inamfaa atulie timu moja kwa muda mrefu

    Jibu

    Maamuzi yako kwake muhusikaa

    Jibu

    Me Kama naona awezi salia

    Jibu

    Hapo anaangalia mkwanja

    Jibu

    kipengele sana hapo city pamoja na mabosi kumpatia fedha za kusajili wachezaj Guadiola hana mengi ya kuifanyia man city kuondoka kwa sasa hitakua wakati mgumu clabuni pale

    Jibu

    Nakukubali sana

    Jibu

    Guardiola anatakiwa atafute maisha mengine

    Jibu

    Uwamuz ni wake

    Jibu

    Kweli kocha Guardiola ameamua msimu huu hataki mchezo akawa lawama kwa kujitia kitazi mwenyewe safii sana neipenda hii

    Jibu

    Vipi unakwama wapi!!

    Jibu

    Maamuzi yake

    Jibu

    afanye maamuz sahh

    Jibu

    Coach mwenye mahesabu

    Jibu

    Kila jambo na wakati wake

    Jibu

    Muda ukifika atasaini

    Jibu

    Uwamuzi anao yy mwenyew

    Jibu

    Uwamuzi anao yy

    Jibu

    Guadiola kama anahtaj kusepa na swala la champion league kama limekuwa kipengele sana hapo city pamoja na mabosi kumpatia fedha za kusajili wachezaj awatakao

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.