Tetesi za Soka Barani Ulaya.


 

Tetesi zinasema Manchester United ina matumaini ya kumsajili winga wa England Jadon Sancho, 20, kutoka Borussia Dortmund kwa kima cha chini ya pauni milioni 100 mwaka huu.

Tetesi zinasema Liverpool imebadilisha msimamo wake kwa ajili ya winga wa Uswisi Xherdan Shaqiri, 29, na haitamruhusu kuondoka mwezi huu.

Kocha mpya wa Paris St-Germain Mauricio Pochettino amehusishwa na kutaka kuwasajili wachezaji wawili waliokuwa Tottenham – kiungo wa kati wa England Dele Alli, 24, na mchezaji wa Inter Milan raia wa Denmark Christian Eriksen, 28.

 

PSG Itawaunganisha Pochettino na Ericksen?

Arsenal imejiunga na vilabu vingine vya Ligi ya Premier ambavyo vimeonesha nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Celtic raia wa Scotland Ryan Christie, 25, ikiwa na matumaini kwamba aliyekuwa beki wa kushoto wa timu hiyo Kieran Tierney, 23, atafanikiwa kumshawishi kiungo huyo kuingia uwanja wa Emirates.

Tetesi zinasema Mikel Arteta hana uhakika ikiwa kiungo wa kati wa Ujerumani Mesut Ozil atarejea kikosini. Mchezaji huyo, 32, hakuchezea Arsenal msimu huu.

Tetesi zinasema AC Milan na Paris St-Germain wanataka kumsajili winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha, 28, katika dirisha hili.

Tetesi zinasema Borussia Dortmund imeonesha nia ya kumchukua winga wa Manchester City, 18, Mholanzi Jayden Braaf.

 

Mlinzi wa Arsenal Rob Holding, 25, anakaribia kufikia makubaliano mapya ya muda mrefu, na kumaliza matumaini ya timu nyingine kubwa kubwa zilizokuwa zinapania kumchukua kwa mkopo.

Tetesi zinasema mchezaji wa USA DeAndre Yedlin, 27, huenda bado akasalia Newcastle msimu huu licha ya mazungumzo ya kuondoka mnamo mwezi huu.

Kocha wa Everton Carlo Ancelotti hata mzuia mchezaji yeyote ambaye anataka kuondoka klabu hiyo mwezi huu lakini anasema hakuna ambaye ameonesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Uturuki, 29, Cenk Tosun.

Juventus inafikiria kumnunua mshambuliaji wa klabu ya Shandong Luneng, Graziano Pelle, 35, aliyewahi kuichezea Italia ambaye pia amehusishwa na West Ham.

Tetesi zinasema Kocha Nuno Espirito Santo anasema Wolves iko tayari kufanya maamuzi kipindi cha usajili wa wachezaji Januari.

Brighton haitarajii kuuza mchezaji yeyote muhimu Januari, licha ya matatizo ya kifedha ambayo yametokana na ugonjwa wa virusi vya corona lakini baadhi ya wachezaji katika kikosi chake huenda wakaondoka kwa mkopo.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Dundee United imewasilisha ombi la kumtaka mchezaji wa klabu ya Airdrieonians, 20, mshambuliaji wa Ufaransa Thomas Robert, ambaye pia amehusishwa na kuhamia Rangers na Celtic.

Tetesi zinasema Wolves inaongoza West Brom na Fulham katika mbio za kutaka kumsajili mlinzi wa Grimsby, 19, Mattie Pollock.

Tetesi zinasema mlinzi wa Aston Villa Bjorn Engels, 26, amehusishwa na kurejea Ubelgiji mwezi huu.

Shirikisho la kandanda (FA) limeonya vilabu kuwa ni lazima vitimize michuano ya raundi ya tatu ya kombe la FA Cup wiki ijayo hata kama wachezaji wanaopatikana na waliothibitishwa kutokuwa na virusi vya corona ni 14 pekee.

 


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?

SOMA ZAIDI

20 Komentara

    Tetesi zinasomeka

    Jibu

    Tetesi ziko poa

    Jibu

    United wakituwekea huyu biashara imeisha ni ushind kila siku

    Jibu

    Zimeeleweka tetesi

    Jibu

    United wajipange

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Sancho. Njoo man

    Jibu

    Asante kwa tetesi bomba meridianbet

    Jibu

    Goodnews

    Jibu

    Tetesi za kukata na shoka

    Jibu

    Itakuwa poa sana kama man u wakifanikiwa kumsajili sancho

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Carlo yuko sahihi

    Jibu

    Tetesi ziko poaa

    Jibu

    Ngoja tuone

    Jibu

    Nice update

    Jibu

    Taarifa timamu

    Jibu

    ngoja tuone

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.