Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Tanzania Bw. Almas Kasongo, amesema kuwa macho yao yote ni kwenye mechi zote ambazo zitachezwa na kuwataka mashabiki pamoja na timu kuzingatia kanuni.
Hivi karibuni kumekuwa na matukio yasiyo ya kinidhamu ambapo mashabiki wamekuwa wakiwapiga waamuzi kwa machupa na wakati mwingine kuingia uwanjani jambo ambalo haliruhusiwi kikanuni.

Suala hilo limekuwa likisababisha adhabu kwa timu husika pale inapobainika tatizo hilo.
Lala salama kumekuwa na matukio mengi ambayo yanahatarisha usalama kwa wachezaji pamoja na waamuzi jambo ambalo kwa sasa linafuatiliwa kwa ukaribu.

Kasongo amesema:”Mechi zote ambazo zimebaki tunazitolea macho na kuzitazama kwa ukaribu, lengo ni kuona kwamba kila kitu kinakwenda sawa na hakuna kinachoharibika.
“Mashabiki, wachezaji na timu kiujumla ni muhimu kuzingatia kanuni ambazo zipo kwani mpira unaendeshwa na kanuni ambazo zipo,”.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.



Venerose
Ni Jambo jema kukiwa na mashabiki ktk mechi za hapa nyumbani
Hopemwaikuka
Itapendeza sana
warda
Hawa nao wanataka pesa tu