Nahodha wa Denmark, Simon Kjaer amesema tukio la Christian Eriksen katika mechi yao ya ufunguzi ya Euro 2020 kuliunganisha kikosi pamoja na kuwasaidia kufika nusu fainali.
Denmark walipata kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Finland katika pambano hilo, ambalo lilicheleweshwa kwa muda mrefu katikati ya mechi hiyo, na walipoteza kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Ubelgiji katika mechi yao iliyofuata. Walakini, waliifunga Urusi ili kufuzu kwa 16 bora, na Wales 4-0 katika 16 bora.

Akiongea baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Jamhuri ya Czech huko Baku, Kjaer alielezea kwamba Denmark hawaridhiki, hata hivyo, kwa kufika hatua nne za mwisho.
Alipoulizwa juu ya athari ambazo ugonjwa wa Eriksen ulikuwa nazo kwenye kikosi, alisema: “Ilibadili jambo kwenye timu. Tuna na tuko salama pamoja. Tunajua tunaweza kuamini watu walio karibu nasi. Tunajua kwamba ikiwa mmoja wetu ana shida, basi mtu mwingine yuko kwa ajili yako.
“Inatupa usalama na kwa kweli inamfanya Christian ajisikie vizuri.
“Tunaweza kushinikiza kwa sababu tunajua kwamba mchezaji aliye karibu nasi yupo na anatuunga mkono.”
Kjaer anaamini timu yake itatinga hatua ya fainali, wakati timu hiyo itakapokutana na England katika mchezo utakao pigwa huko Wembley.
IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!

