Refa wa kimataifa wa Tanzania, Ramadhan Kayoko ni miongoni mwa waamuzi tisa wa kati walioteuliwa na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Refa huyo ameteuliwa kuchezesha mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 23 (CECAFA U23) yatakayofanyika Ethiopia kuanzia Julai 18 hadi 31.
Kayoko mwenye beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), ataungana na marefa wengine wa kati kutoka nchi nane kushika kipyenga katika mashindano hayo yanayofanyika kwa mara ya kwanza kwenye ukanda huu.
Mbali na Kayoko, Tanzania pia imetoa refa msaidizi katika mashindano hayo ambaye ni Kassim Mpangwa aliye pia na beji ya FIFA.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


