Klopp Anena Kuwashindwa Leicester!

Wiki hii Ligi Kuu ya Uingereza imeshuhudia baadhi ya watabe wa EPL wakiwa na wiki ngumu, Liverpool wameshindwa kupata ushindi wakiwa wenyeji wa Leicester City kwenye gemu ya jana, Klopp anena sababu ya kuwashindwa Leicester City.

Wakati Manchester United wakiponea chupu chupu kwa kulazimisha sare ya bao 2-2 dhidi ya Burnley usiku wa Januari 29, Manchester City alikubali kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa Newcastle United. Januari 30 imekuwa mbaya zaidi kwa Chelsea aliyechapwa bao 4-0, huku Liverpool akimaliza kwa kuruhusu sare ya bao 1-1.

Akielezea kwa nini Liverpool wameshindwa kuwachapa Leicester City wakiwa kwao, meneja Jurgen Klopp anasema kuwa Barafu iliyoanguka uwanjani humo ilikuwa ni moja ya sababu iliyopelekea ugumu wa gemu dimbani na kujikuta wakimaliza kwa sare kwenye gemu hiyo.

Klopp pia amegusia makosa ambayo anaamini yangekuwa yamebadilisha matokeo kama vile kunyimwa penati wakati kulikuwa na rafu aliyochezewa Keita na Pereira.

Leicester wamebahatika kuwa timu ya pili kuondoka bila kichapo pale Anfield msimu huu baada ya Man City kufanya hivyo oktoba 7 mwaka uliopita. Hata hivyo Liverpool wanaendelea kuwa vinara wakitofautana kwa pointi 5 na timu inayowafuatia Manchester City.

2 Komentara

    Leicester wanajua

    Jibu

    klopp yuko vizuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.