Cassano Amemchana Mkewe Icardi

Kumekuwa na stori kibao kuhusu hatma ya Mauro Icardi klabuni Inter Milan na kuhushwa kwake na vilabu mbalimbali. Mkewe Icardi Wanda Nara ambaye pia ni wakala wa mchezaji huyo ameonekana kuwa na mchango mkubwa zaidi katika hali inayoendelea juu ya uhusiano wa nyota huyu na klabu yake.

Antonio Cassano mara ya kwanza Antonio Cassano alimshambulia mwanamama huyo kuwa ndiye sababu ya mmewe kuvuliwa ukapteni klabuni hapo. Cassano alizungumza kwenye kipindi cha Tiki Taka, na hajataka kupepesa macho kuzungumza tena tuhuma zake mbele yake.

Staa huyu wa zamani, ambaye anaiita hali inayoendelea juu ya uhusiano wa Icardi na Klabu yake kuwa ni janga anasisitiza kuwa ni janga ambalo limetengenezwa na Nara, amemshauri Nara amwambie mmewe aombe msamaha kwa wanatimu wenzake kabla hali ya hewa haijawa mbaya zaidi.

Cassano anasema kuwa tatizo la mke wa Icardi ni kuwa anaongea sana na anatumia vibaya mitandao ya kijamii. Bwana huyu amesisitiza kuwa kuvuliwa kwa unahodha kwa Icardi kusingetokea bila sababu kwa kuwa Ausilo, Marotta, Spalletti na Zhang sio vichaa isipokuwa mwanamama huyu anatumia mitandao vibaya kumharibia mme wake.

Makala iliyopita

5 Komentara

    Icardi mwenyew mpole sana #Meridianbettz

    Jibu

    Ukiwa star shida kweli

    Jibu

    Hatari sana.

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.