Lukaku : Sifurahi na Hali ya Chelsea, Nitarejea Inter.

 

Mshambuliaji wa Chelsea, Romelu Lukaku amefunguka na kuweka wazi kutofurahishwa na mfumo unaotumika na meneja wake Thomas Tuchel ndani ya klabu hiyo.

 

Lukaku ameenda mbali zaidi na kusema hana furaha ndani ya klabu hiyo na ipo siku atarejea katika klabu ya Inter Milan kwani anajutia jinsi gani aliondoka ndani ya klabu hiyo.

” Utimamu wa kimwili nipo sawa . Lakini sina furaha na hali ilivyo ndani ya Chelsea. Tuchel ameamua kucheza na mfumo mwingine – sitokata tamaa , nitakuwa professional, sina furaha na hali ilivyo lakini nitakuwa professional na siwezi kukata tamaa sasa . “ alisema Lukaku.

“ Ni matumaini yangu kutoka moyoni kabisa kurejea tena Inter Milan tena sio mwisho wa maisha yangu ya soka bali bado nikiwa katika ubora wangu ili kutwaa zaidi mataji pamoja .

“Nataka kuomba msamaha kwa mashabiki wa Inter , muda ambao niliongea maneno yangu haukuwa muda sahihi , mulichonifanyia kitabaki milele kwenye moyo wangu “

“ Huu ni muda sahihi wa kushea hisia zangu , mara zote huwa nasema Inter ipo moyoni mwangu , najua nitarejea Inter Milan , naipenda Italia , huu ni muda sahihi wa kuongea na kuwafahamisha watu nini kilitokea “

“ Nafikiri kila kitu kilichotokea majira ya kiangazi yaliyopita , haikutakiwa kutokea kama vile …jinsi nilivyoondoka Inter , namna nilivyoondoka klabuni , jinsi nilivyowasiliana na mashabiki …inanisumbua kwasababu haikuwa muda sahihi “ aliongeza.


KUWA MILIONEA MSIMU WA SIKUKUU NA SAHARA RICHIES

Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.