Sevilla wamedhamiria kumsajili Anthony Martial kutoka Manchester United katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari kwa mujibu wa chanzo cha Kihispania cha Cope.
Vilabu vyote viwili bado viko tofauti kwa kiasi fulani katika muundo wa kifedha wa mpango huo, lakini inaeleweka kuwa mchezaji mwenyewe amedhamiria kuondoka Old Trafford.
Sevilla wanatarajiwa Kuweka mambo yao sawa kwa siku zijazo na kuyafikia mahitaji ya United huku Monchi akiona kuwa ni muhimu kupata mshambuliaji mwingine Sevilla.

Klabu hiyo ya Andalusia inamaliza mwaka ikiwa nafasi ya pili kwenye La Liga, pointi nane nyuma ya vinara Real Madrid huku wakiwa na mchezo mkononi.
Kusajili mfungaji kutaimarisha ubora wao, wakati Youssef En-Nesyri amejeruhiwa na anatazamiwa kutinga fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika akiwa na Morocco huku Rafa Mir akiwa hajaonesha uwezo mkubwa.
Martial, 26, amechangia mabao 79 na asisti 50 katika mechi 268 alizoichezea United. Amecheza mechi kumi pekee msimu huu akifunga mara moja katika dakika 359 za soka.
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

