Kikosi cha Simba SC kimewasili salama jijini Dar es Salaam jana mchana kutoka nchini Morocco baada ya majukumu ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi kukamilika.

Baada ya kufika Dar wachezaji wameruhusiwa kwenda kuziona familia zao na leo watarajea mazoezini kujiandaa na mechi ya Ligi Kuu ya NBC itakayopigwa Ijumaa Machi 4, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku dhidi ya Biashara United.
Mechi hiyo ya Simba SC ni muelendelezo wa ligi ya NBC ambapo itaanza rasmi mzunguko wa pili.
Katika mchezo huo Simba SC inatarajia uwepo wa baadhi ya wachezaji ambao walikuwa majeruhi na kuikosa mechi kadhaa ambao watakuwa wamepona na wako fiti.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


