Klabu ya Mamelodi Sundowns imezidi kuendeleza ubabe wake kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa baada ya kumchapa Cotton Sport hapo jana kwa mabao 3-1 alipokuwa ugenini.
Hivyo baada ya ushindi huo Mamelodi anafikisha pointi 6 kwa kushinda michezo yake yote miwili na kuongoza Kundi B.
Mabao hayo yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza cha mchezo huku kipindi cha pili kikimalizika bila kufungana bao lolote.
Wakati kwa upande mwingine Wababe wa Misri Al Ahly ambao nao wapo kundi hilo hilo watamenyana dhidi ya Al Hilal Omdurman ya Sudan ambao wao walipoteza mechi yao ya kwanza.