Klabu ya Wydad Casablanca ambaye ndiye bingwa mtetezi wa Kombe hili ameshindwa kufurukuta hapo jana dhidi ya JS Kabylie kwa bao 1-0 alipokuwa ugenini.

Wydad ambaye kwenye Ligi ya Morocco yupo nafasi ya pili akiwa na pointi zake 32 alitarajia kupata ushindi ugenini ili ajiweke kwenye nafasi nzuri kwenye michuano hii lakini haikuwa hivyo.
JS Kabylie ya Algeria ilizima ndoto za bingwa mtetezi huyo ambapo bao la kuizamisha timu hiyo lilifungwa dakika ya 87 ya mchezo jioni kabisa na kuifanya klabu hiyo kushindwa kusawazisha bao hilo wakijipa matumaini mechi ijayo.

Mechi inayofuata ya Klabu bingwa barani Afrika atamenyana dhidi ya Petro Atletico kusaka pointi tatu muhimu ili aweze kusalia katika michuano hiyo.

