Croatia watalazimika kucheza bila mchezaji wao Ivan Perisic ambaye amepata maambukizi ya Korona pindi watakapocheza dhidi ya Spain kesho usiku katika mechi ya hatua ya kumi na sita bora.
Ivan Perisic ambaye amefunga magoli mawili katika mechi mbili kati ya tatu na kuisaidia timu yake kuingia hatua ya 16 bora atalazimika kujitenga na wenzake kwa siku 10 akiwa chini ya uangalizi maalum.

Perisic ni miongoni mwa wachezaji muhimu wa Croatia na ukosefu wake kwenye kikosi cha Croatia kunaweza kuwa pigo, hususan pale ambapo wanaenda kukutana na Spain ambayo imeshinda kwa goli 5-0 dhidi ya Slovakia katika kuingia 16 bora.
Shirikisho la soka la Croatia lilipokea taarifa ya vipimo vya wachezaji wa Croatia na kugundua kuwa Ivan ana Korona hivyo atalazimika kukaa nje kujitenga na wenzake kwa siku 10 na kutoruhusiwa kucheza mechi yoyote.
Hakuna mipaka ya ushindi kwenye Keno Instant ya meridianbet Kasino, hii wewe ndiyo una uamuzi zaidi juu ya mchezo na nafasi ya machaguo kibao.


