Kocha wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez amesisitiza kuwa kiungo wake huyo wa kimataifa kutoka uholanzi Frenkie de Jong atakuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi hicho ikiwa ataamua kubaki Nou Camp.
Xavi alishakubali kuwa swala Frenkie de Jong liko nje ya uwezo wake, kutokana na mchezaji mwenyewe kutoeleweka kwenye maswala ya mshahara wake, kwani yeye ni miongoni mwa wachezaji wanaolipwa pesa ndefu na timu inatafuta unafuu wa kifedha

“Frenkie de Jong sio mchezaji wa kuanzia nje, yeye ni mchezaji muhimu na nimeshasema mara nyingi. Sijui nini kitatokea, lakini ikiwa atasalia ataendelea kuwa mchezaji muhimu.” Alisema Xavi baada ya mchezo wo dhidi ya Rayo Vallecano kuisha kwa sare ya kutokufungana.
Frenkie de Jong kwenye mchezo dhidi ya Rayo Vallecano siku ya jumamosi aliingia akitokea benchi na kuchukua nafasi ya Gavi.

