Kocha wa Tottenham Hotspur FC, Igor Tudor, amethibitisha kuwa uamuzi wa kumtoa mlinda mlango Antonín Kinský katika mchezo dhidi ya Atlético Madrid ulikuwa sahihi, baada ya kipigo cha mabao 5-2 katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ya UEFA Champions League uliofanyika Uwanja wa Metropolitano Stadium.

Kinský alibadilishwa dakika ya 17 ya mchezo baada ya kuonesha dalili za mkanganyiko, baada ya kupokea mabao matatu ndani ya dakika 15 za mwanzo, ikiwa ni pamoja na kushindwa kuondoa mpira kwa bao la kwanza na kufanya kosa la kumchezesha mpira vibaya katika bao la tatu.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Tangu kabla ya mchezo, uamuzi huo ulikuwa sahihi kuzingatia wakati tulipo,” alisema Tudor kwenye mkutano na waandishi wa habari, akirejelea uamuzi wake wa kumtumia Kinský mwenye umri wa miaka 22 badala ya mlinda mlango wa kawaida Guglielmo Vicario. Kwa sasa tuko katika wakati mgumu, tuko dhaifu,”

Kinski alikuwa akicheza mchezo wake wa kwanza tangu Oktoba na mchezo huu ulikuwa wa tatu tu kwake msimu huu, hali iliyoongeza changamoto kwa Tudor ambaye amepoteza michezo minne yote tangu alipochukua nafasi ya kocha mkuu Februari mwishoni mwa mwezi uliopita.
Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone, na washambuliaji wake wameendelea kuonyesha uwezo mkubwa, huku Julián Álvarez akifunga mabao mawili na kudokeza kuwa timu yao inajua umuhimu wa kila kipengele katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa.

“Tunajua mashindano haya ni magumu. Kila jambo dogo lina umuhimu. Haitakuwa rahisi, lakini tunataka kufika robo fainali,” alisema Álvarez kuhusu mchezo wa pili utakaochezwa London wiki ijayo.

