Kane Anafikia Rekodi ya Henry

Mshambuliaji wa timu ya Tottenham Spurs na timu ya taifa ya Uingereza Harry Kane anafikia rekodi ya Thierry Henry ya kufunga mabao mengi zaidi katika mechi za dabi za ligi kuu ya Uingereza ambapo Spurs aliichakaza Fulham kwa mabao 2-1.

Kane Anafikia Rekodi ya Henry

Goli la kwanza la Spurs lilifungwa na Pierre-Emile Hojbjerg katika kipindi cha kwanza na golikipa wa zamani wa Arsenal Ben Leno aliweka alama ya heshima kwa kuokoa mipira kadhaa ambayo alipigiwa.

Kane aliweza kuongeza faida kwa Spurs mara mbili baada ya kufunga bao hilo akiwa karibu na goli, huku bao hilo likimchukua nafasi ya tatu kwenye orodha kwenye wafungaji wa muda wote wa shindano hilo la dabi. Wakati kwa upande wa Fulham bao lao lilifungwa na Aleksandar Mitrovic ambaye anafunga mechi ya nne mfululizo.

Kane Anafikia Rekodi ya Henry

Harry Kane alipachika bao lake la 43 la ligi kuu ya Uingereza katika mchezo wa dabi ya London, mechi sita msimu huu Spurs hawajapoteza mchezo wowote huku wakitoa sare moja tu, huku wakishinda mechi zao tatu za ufunguzi za nyumbani.

 

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.