Mshambuliaji wa timu ya Tottenham Spurs na timu ya taifa ya Uingereza Harry Kane anafikia rekodi ya Thierry Henry ya kufunga mabao mengi zaidi katika mechi za dabi za ligi kuu ya Uingereza ambapo Spurs aliichakaza Fulham kwa mabao 2-1.

Goli la kwanza la Spurs lilifungwa na Pierre-Emile Hojbjerg katika kipindi cha kwanza na golikipa wa zamani wa Arsenal Ben Leno aliweka alama ya heshima kwa kuokoa mipira kadhaa ambayo alipigiwa.
Kane aliweza kuongeza faida kwa Spurs mara mbili baada ya kufunga bao hilo akiwa karibu na goli, huku bao hilo likimchukua nafasi ya tatu kwenye orodha kwenye wafungaji wa muda wote wa shindano hilo la dabi. Wakati kwa upande wa Fulham bao lao lilifungwa na Aleksandar Mitrovic ambaye anafunga mechi ya nne mfululizo.

Harry Kane alipachika bao lake la 43 la ligi kuu ya Uingereza katika mchezo wa dabi ya London, mechi sita msimu huu Spurs hawajapoteza mchezo wowote huku wakitoa sare moja tu, huku wakishinda mechi zao tatu za ufunguzi za nyumbani.

