Kocha msaidizi wa timu ya wananchi Cedric Kaze amewataka wachezaji wa timu yake kutowadharau Rhino Rangers ya mkoani Tabora kwenye mchezo wa leo hatua ya 32 ya kombe la Shirikisho la Azam katika uwanja wa Mkapa jioni. Odds kubwa za soka unazipata Meridianbet.

Kaze alisema kuwa wachezaji wa timu kubwa huwa na tabia ya kudharau mechi ndogo, hivyo hucheza kwa kiwango cha chini tofauti na mechi za kwenye ligi kuu.
Hata hivyo kuelekea kwenye mchezo huo Kaze, amewakumbusha tu nyota wa Yanga kwamba kwenye mashindano hayo ili ufike fainali ni lazima kuifunga kuifunga kila timu. Ukiwa na meridianbet unaweza kubashiri mubashara, tembelea maduka ya meridianbet uweze kubashiri.
Kwa upande wa Rhino Rangers timu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kocha mkuu wa timu hiyo Athumani Bilali alisema kuwa haiyogopi Yanga bali anaiheshimu kwakuwa ni klabu kubwa.

“Siwaogopi Yanga nimekutana nao mara nyingi zaidi kwenye michezo ya ligi kuu na kuwafunga, hivyo leo tunawaheshimu timu ya Wananchi ila sisi ni wenye nchi” Kocha Mkuu wa Rhino
Mshindi wa mchezo huo atafuzu moja kwa moja kuingia hatua ya 16 bora, na kuungana na timu nyingine zilizofuzu hatua hiyo ambazo ni Simba SC, Mbeya City, KMC, African Sports na Singida BS. Meridianbet wanatoa ODDS kubwa kwenye mechi zote. Bashiri hapa.

