BAADA ya kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Hilal Al Sahil kwa bao 1-0, hatimaye Geita Gold wamerejea Dar kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa marudiano.
Kikosi hicho kesho jumatano kitacheza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida Big Stars huku jumamosi ikitarajia kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Hilal Al Sahil ya Sudan.
Mchezo huo wa marudiano utapigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar ambapo ili Geita waweze kuvuka hatua hiyo wanapaswa kushinda mabao 2-0.
Akizungumzia hilo, Ofisa Habari wa Klabu hiyo, Hemed Kivuyo amesema kuwa “Kikosi tayari kimerejea Dar kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya Singida Big Stars.
View this post on Instagram
“Wachezaji ambao hawakwenda na timu nchini Sudan tayari wameungana na wenzao kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa marudiano dhidi ya Hilal Al Sahil.”