Kocha Mpya Anukia Simba

Klabu ya Simba ipo mbioni kumalizana na na kocha wa klabu ya Horoya ya nchini Guinnea, Kocha huyo ambaye ni raia wa Senegal Lamine N’diaye.

Viongozi wa klabu ya Simba wako katika hatua za mwisho mwisho kukamilisha dili la kumshusha kocha huyo mwenye uzoefu na soka la Afrika, Inaelezwa kocha huyo anatakiwa kuungana na timu hiyo kuelekea michuano ya Mapinduzi nchini Zanzibar.SIMBAKocha huyo atakuja kuungana na kocha wasasa klabuni hapo Juma Mgunda na yeye atasimama kama kocha mkuu, Huku Mgunda akisimama kama kocha msaidizi kutokana na uzoefu mkubwa aliokua nao Lamine.

Kocha Lamine N’diaye ambaye amewahi kuvifundisha vilabu vya Tp Mazembe, Al Hilal, Pamoja na timu ya taifa ya Senegal na kwasasa akifanikiwa kuifanya Horoya kua moja ya vilabu tishio barani Afrika.SIMBAKocha huyo mwenye uzoefu mkubwa na soka la Afrika anakuja ndani ya klabu ya Simba kwajili ya kuliongezea nguvu benchi la ufundi la klabu hiyo kuelekea ligi ya mabingwa Afrika, Ambapo klabu hiyo ipo kwenye hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.