Nyota wa kikosi cha Geita Gold, Saido Ntibazonkiza ataukosa mchezo ujao wa ligi baada ya kupewa kadi nyekundu.

Mchezaji huyo alipewa kadi hiyo jana kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo mtanange huo ulimalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Kadi nyekundu ya Ntibazonkiza ilitokana na faulo aliyomchezea nyota wa Mtibwa Sugar, Omar Sultan dakika ya 54 ya mchezo.
Mabao ya Geita Gold kwenye mchezo huo yalifungwa na Ntibazonkiza kwa mkwaju wa pelnati na Juma Luizio.

Mabao ya Mtibwa Sugar yalifungwa na Juma Nyangi huku bao la pili likiwa la kujifunga kutoka kwa beki wa Geita Gold George Wawa.


