Saido Ntibazonkiza Alamba Mkataba Geita Gold wa Miaka 2

RASMI uongozi wa Geita Gold umemalizana na aliyekuwa nyota wa Yanga, Saido Ntibazonkiza kwa mkataba wa miaka miwili.

Ntibazonkiza alimaliza mkataba wake na Yanga mwishoni mwa msimu uliopita ambapo timu hiyo chini ya Kocha Mkuu, Nassredine Nabi haikumuongezea mkataba.

Akizungumzia usajili huo, Ofisa Habari wa Geita Gold, Hemed Kivuyo amesema kuwa “Ni kweli tumemalizana na Saido kwa mkataba wa miaka miwili.

“Tumechelewa kumtangaza kutokana na makubaliano ya muda mrefu tuliyokuwa nayo ambapo hatukuafikiana lakini kwa sasa ni mchezaji wetu.” 

Kutokana na uzoefu mkubwa alionao Saido kwenye mashindano mbalimbali utaisaidia Geita Gold hasa kwenye michuano ya Shirikisho barani Afrika ambapo timu hiyo itashiriki.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.