INAELEZWA kuwa, uongozi wa Simba umefikia makubaliano ya kumrudisha aliyekuwa kocha wa makipa wa timu hiyo, Mbrazil, Milton Nienov ambaye kwa sasa yupo Yanga akimaliza mkataba wake. Tembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa.
Taarifa zisizo na shaka zinadai kuwa, viongozi wa Simba wameshakubaliana kila kitu na kocha huyo, walikuwa wanasubiri jana Yanga wamalizane na Azam FC katika fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports, ili kukamilisha jambo hilo. Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.
“Ni kweli kuna maboresho makubwa ya benchi la ufundi kwa kuondolewa baadhi waliopo na kuletwa wapya kuja kuungana na Kocha Mkuu, Roberto Oliveira ‘Robertinho’ ambaye amewapendekeza kuja kufanya nao kazi,” kilisema chanzo makini.
Ukiwa na meridianbet unapata odds kubwa, kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti.
Ikumbukwe tayari Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Gain’, alishaweka wazi juu ya suala la kuboresha benchi la ufundi la timu hiyo kwa kusema wanayajua makosa waliyofanya msimu huu, hivyo wamejipanga kufanya maboresho makubwa msimu ujao. Pata odds kubwa kutoka Meridianbet kwa mechi za ligi mbalimbali.