Klabu ya Simba imefunga usajili hapo jana kwa kumtambulisha Jean Baleke anayecheza katika nafasi ya ushambuliaji kutoka Taifa la DRC Congo.
Mnyama imemtambulisha mchezaji huyo ikiwa ni usajili wa tatu kuufanya dirisha hili ambapo mcezaji huyo ataenda kuungana na kina Bocco Kyombo na wengine katika eneo la ushambuliaji.
Jean Baleke amewahi kucheza katika klabu mbalimbali zikiwemo JS Kinshasa ya Congo, TP Mazembe, pamoja na Nejmeh SC ya Lebannon na sasa ametua Msimbazi kuja kuonyesha kiwango alichonacho.
Mshambuliaji huyo anacheza pia timu ya Taifa ya Congo chini ya umri wa miaka 23 kwani anaripotiwa kuwa na miaka 21, lakini pia anakiwasha katika timu ya Wakubwa.