Yanga Yatinga Fainali ya Afrika Kibabe

Klabu ya Yanga imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya kombe la shirikisho Afrika kibabe baada ya kuifumua klabu ya Marumo Gallants kwa mabao mawili kwa moja katika uwanja wake wa nyumbani.

Yanga wamefanikiwa kutinga fainali ya Afrika ikiwa ni mara yao ya kwanza kwenye historia ya klabu hiyo baada ya kupata ushindi kwenye mikondo yote miwili ya hatua ya nusu fainali, Wananchi walifanikiwa kushinda kwa mabao mawili kwa bila mchezo uliomalizika na kufanikiwa kurudia walichokifanya wiki iliyopita.YangaKocha Nassrdine Nabi alikwenda na mkakati uleule ambao ulimpatia matokeo katika dimba la Benjamin Mkapa Jumatano iliyopita, Kuwaruhusu Marumo kukaa na mpira halafu wao wanatumia mipira ya kushtukiza na karata hiyo imefanikiwa tena leo nchini Afrika Kusini.YangaMabao ya Fiston Kalala Mayele kipindi cha kwanza na Kenedy Musonda yameiwezesha Yanga kutinga fainali kibabe kwa jumla ya mabao manne kwa moja, Huku Fiston Kalala Mayele akiwa nyota wa mchezo kwani amekua na kiwango bora sana baada ya kufunga baoa moja na kupiga pasi ya bao kwenda kwa Kenedy Musonda.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.