AC Milan yaazimia kumrudisha Federico Chiesa Serie A msimu huu wa kiangazi baada ya muda mfupi akiwa Liverpool, kwa mujibu wa ripoti kutoka Italia.

Winga huyo alishinda taji la Ligi Kuu ya England (Premier League) katika msimu wake wa kwanza, lakini alicheza mechi 14 pekee za mashindano akiwa na klabu hiyo kutokana na majeraha na kushuka kwa kiwango.
Hata hivyo, aliweza kuchangia mabao mawili, lakini sasa anatafuta muda zaidi wa kucheza ili arejee kwenye kiwango bora na kuingia tena kwenye kikosi cha Italia kuelekea Kombe la Dunia la 2026.
Kwa mujibu wa ripota wa DAZN, Orazio Accomando, Milan inapanga kutoa pendekezo la mkopo lenye chaguo la kumnunua Chiesa msimu huu wa kiangazi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ni zao la akademia ya vijana ya Fiorentina na aliondoka Juventus kwa €12 milioni pamoja na bonasi msimu uliopita wa kiangazi, baada ya Bianconeri kushindwa kumpa mkataba mpya.


