Klabu ya Arsenal leo itashuka dimbani kumenyana na klabu ya Manchester United katika mchezo wa kirafiki ambao pia ni maalumu kwa maandalizi ya kuelekea msimu ujao wa 2023/24.
Arsenal baada ya kucheza michezo yake miwili na kufanikiwa kupata ushindi mchezo mmoja na kusuluhu mchezo mmoja wanaenda kumenyana na Man United ambao mpaka sasa wamefanikiwa kushinda michezo yao yote miwili ya kirafiki.
Mtanange huo ambao utapigwa nchini Marekani ambapo timu hizo zipo kwajili ya maandalizi yao kuelekea msimu ujao, Mchezo huu umevuta hisia za mashabiki sana haswa ukizingatia ni moja ya vilabu hasimu zaidi kutoka nchini Uingereza na vina mashabiki wengi.
Kuelekea mtanange huu kati ya Arsenal na Man United kocha wa klabu ya United Erik Ten Hag jana akiongea na wanahabari alisema kwao mchezo huu hawatauchukulia kama wa kirafiki bali watakwenda kucheza kama mchezo muhimu kwao.
Mchezo huu unatarajiwa kua na mvuto na mgumo licha ya kua wa kirafiki kwani kauli ya kocha Ten Hag imeshaonesha kua wameutafsiri mchezo huu kwa namna gani na kwa upande wa Arsenal nao hawatauchukulia mchezo huu kiuwepesi kutokana na uhasimu uliopo baina ya vilabu hivi.

