Mchezaji wa Inter Milan, Ashley Young anaendelea kugonganisha vichwa vya viongozi wa vilabu mbalimbali. Uzoefu wake kwenye soka ni lulu inayowaniwa.
Imeripotiwa kuwa wakala wa Young yupo mazungumzoni na uongozi wa Aston Villa kuhusu uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo kwa mkataba wa mwaka mmoja (wenye uwezekano wa kuongeza mwaka mmoja zaidi).
Ukiachilia mbali Villa, Young anahusishwa na Watford, Burnley pamoja na Inter wenyewe ambao wanampango wa kumuongezea mkataba wa mwaka mmoja.
Young aliwahi kuitumikia Aston Villa kwa muda wa miaka minne na nusu na inasemakana huenda Ashley Young akavutiwa zaidi na kurudi Villa Park kuliko kwenda kwenye klabu nyingine.
SHINDA TSH 150,000,000/=
Mtaani kumechangamka, washkaji wanakamata mkwanja kwa mkakati tu na Footbal Fever! Ni rahisi, changamkia fursa hii kushinda mgao wako wa TSH 150,000,000/= 💰🤑


