Aubameyang Avunja Rekodi Wembley.


Pierre-Emerick Aubameyang alifunga penalti ya ushindi na kuwaongoza Arsenal kunyanyua ubingwa wa Community Shield baada ya kuwaangusha Liverpool 5-4 kwenye mechi iliyowakutanisha ugani Wembley, Uingereza mnamo Agosti 29, 2020.

Mshindi wa mechi hiyo aliamuliwa kupitia penalti baada ya pande zote kuambulia sare ya 1-1 mwishoni mwa muda wa dakika 90.

Arsenal ndio waliokuwa wa kwanza kuliona lango la Liverpool kupitia goli la Aubameyang kunako dakika ya 12 kabla ya chipukizi Takumi Minamino kusawazishia Liverpool katika dakika ya 73.

 

Aubameyang Avunja Rekodi Wembley.

 

Bao la Minamino ambalo lilikuwa lake la kwanza kambini mwa Liverpool, lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na mshambuliaji matata mzawa wa Misri, Mohamed Salah.

Ingawa Arsenal walilalamikia refa kwamba bao hilo lilifumwa wavuni na Minamino baada ya Salah kunawa mpira, teknolojia ya VAR ilibainisha vinginevyo.

Huu ni mwaka wa pili mfululizo kwa Liverpool kupoteza ubingwa wa Community Shield kupitia penalti. Mwanzoni mwa msimu wa 2019-20, Liverpool walizidiwa maarifa na Manchester City kwa mikwaju 5-4 ya penalti uwanjani Wembley.

Aubameyang alidhihirisha umuhimu wake kambini mwa Arsenal ambao kwa sasa wanatiwa makali na kocha Mikel Arteta.

 

Aubameyang Avunja Rekodi Wembley.

Nyota huyo mzawa wa Gabon alifunga tena mabao mawili mnamo Agosti 1, 2020 na kusaidia Arsenal kuwabwaga Chelsea 2-1 ugani Wembley. Ushindi huo wa Arsenal uliwanyanyulia ubingwa wa Kombe la FA msimu huu wa 2019-20.

Ushirikiano mkubwa kati ya Aubameyang, Bukayo Saka na Ainsley Maitland-Niles ulitatiza pakubwa mabeki wa Liverpool ambao walishuhudia safu yao ya ulinzi ikivuja kupitia chipukizi Neco Williams.

Na baada ya kila kikosi kupiga jumla ya penalty nne, Aubameyang aliendea mkwaju wa mwisho kwa upande wa Arsenal na kumzidi maarifa kipa matata wa Liverpool, Alisson Becker.

 

Aubameyang Avunja Rekodi Wembley.

Aubameyang anajivunia kufungia Arsenal jumla ya mabao 71 kutokana na mechi 110 zilizopita, na hakuna mwanasoka yeyote katika historia ya Arsenal amewahi kufunga zaidi ya idadi ya magoli matano ambayo yamefungwa na Aubameyang uwanjani Wembley.

Mnamo Agosti 28, Arteta alikiri kwamba Aubameyang alikuwa pua na mdomo kutia saini mkataba mpya kambini mwa Arsenal.

Baada ya kutia kapuni mataji mawili chini ya kipindi cha mwezi mmoja, Arsenal watakuwa wamefunga rasmi kampeni za msimu huu ambao ni wa kwanza chini ya Arteta.

Ingawa Liverpool walikosa huduma za beki Trent Alexander-Arnold na kiungo Jordan Henderson, kocha Jurgen Klopp aliwajibisha kikosi ambacho kilikuwa na wanasoka waliokuwa na uwezo wa kuwapepeta Arsenal ambao pia walikosa maarifa ya mafowadi Nicolas Pepe na Alexandre Lacazette.


Beti Mbio za Mbwa Mubashara

Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.

Cheza Hapa

60 Komentara

    Habari njema.

    Jibu

    Hongera kwake Aubameyang🤝🤝🤝🤝

    Jibu

    Kazi nzuri sana aliifanya aubameyang

    Jibu

    Asante kwa makala meridian

    Jibu

    Arsenal walikuwa on fire hope msimu huu ni wao

    Jibu

    Kazi nzuri

    Jibu

    Mwanzo mzur wa msim

    Jibu

    Asante kwa makala mzur

    Jibu

    Gud newz

    Jibu

    Hongera Sana aubamayang

    Jibu

    Aubameyang yupo vizuri

    Jibu

    Aubameyang anatisha.

    Jibu

    Hatari sana kijana,pongez kwake!!!

    Jibu

    pongezi kwake

    Jibu

    Aubameyang amedhihirisha kwamba aendelee kusalia Arsenal na kuipa mafanikio#meridianbettz

    Jibu

    Asante meridianbet kwa makala hii

    Jibu

    Aubakeyang amefanya kazi nzuri

    Jibu

    Hongera yake

    Jibu

    Hatari sana pongezi kwake

    Jibu

    Ongera Sana Aubameyangu alinifurahisha Sana kupiga mkwaju wamwisho ndio ulio wanyanyua Arsenal

    Jibu

    pongezi kwake

    Jibu

    Aubameyang anawapa sana Raha Arsenal

    Jibu

    Aubameyang katishaa sana

    Jibu

    Safi sana mchezaji mzuri

    Jibu

    Inapendeza

    Jibu

    Hongera kwake Aubameyang#Meridianbettz

    Jibu

    Pongezi kwake Aubameyang

    Jibu

    Hongera aubameyang endelea kupambana

    Jibu

    auba anauwezo mkubwa sana akipata watu wa kumpa pas za mwisho.

    Jibu

    Aubameyang ndio Star pale arsenal kwa moto walianza nao arseno si wamchezo mchezo

    Jibu

    Hongera zake

    Jibu

    vzr

    Jibu

    Aubemeyang yupo vizuri sana

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Ongera arsenal

    Jibu

    Anastahil pongez

    Jibu

    Arteta ndoo ya kwanza

    Jibu

    Amefanya kazi nzuri pongezi kwake.

    Jibu

    Aubameyang jana ameoshenya yeye ni kiungo mzuri na bora wakati wote

    Jibu

    Yuko vizuri anastahili pongezi@meridianbettz

    Jibu

    Hngr zake

    Jibu

    Pongezi sana arsenal mana mmefanya kazi nzuri

    Jibu

    Aubameyang amejua kujitengenezea jina ndani arsenal

    Jibu

    Hongera yake

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Hongera sana kwao#Meridianbettz

    Jibu

    Namkubali sana huyu jamaa

    Jibu

    uyu jamaa lile goli lake lilikuwa balaa sana

    Jibu

    Pongezi kwao

    Jibu

    Tunatengemea mengi mazur kutoka kwake aubemayang

    Jibu

    Auba ni moto anaipa the gunners matokeo muhimu katika mechi muhim

    Jibu

    Kazi mzur auba

    Jibu

    Aubameyang fundi wa mpira.

    Jibu

    Pongezi kwa arsenal.

    Jibu

    Huu ni mwaka wa pili mfululizo kwa Liverpool kupoteza ubingwa wa Community Shield kupitia penalti. Mwanzoni mwa msimu wa 2019-20, Liverpool walizidiwa maarifa na Manchester City kwa mikwaju 5-4 ya penalti uwanjani Wembley.

    Jibu

    Aubameyang amedhihirisha kwamba aendelee kusalia Arsenal na kuipa mafanikio

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.