Mikel Arteta amethibitisha kuwa nahodha Pierre-Emerick Aubameyang ameachwa nje ya kikosi kitakachocheza Jumamosi ya Ligi Kuu dhidi ya Southampton kutokana na sababu za kinidhamu.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 amekuwa akiingia na kutoka kikosini msimu huu msimu huu, huku kukiwa na uvumi juu ya mustakabali wake. Staa huyu hajafunga bao kwenye Ligi Kuu tangu Oktoba 22.

Aubameyang alicheza kwa dakika tano pekee dhidi ya Everton mara ya mwisho, akipoteza nafasi ya pekee kupata pointi kwa timu yake, na ameachwa kwenye kikosi kinachoingia dimbani dhidi ya Southampton.
Arteta alithibitisha kwamba kuachwa kwa nahodha huyo kunatokana na utovu wa nidhamu, huku staa huyo pia akiripotiwa kukosa kuwepo mazoezini siku ya ijumaa.
“Kwa bahati mbaya kutokana na utovu wa nidhamu. Nadhani tumekuwa na msimamo thabiti kwamba tuna baadhi ya wasioweza kujadiliwa kwenye timu ambao tumejipanga kama klabu, na hatacheza leo”
Unaweza kujishindia mamilioni katika kasino yako pendwa ya meridianbettz, mchezo wa Agent Jane Blonde Return ni moja ya michezo inayopendwa kwasasa huku ikiwafanya wachezaji kuwa mamilionea kila siku. Unasubiri nini! ungana na Agent Jane Blonde akufanye milionea.
CHEZA HAPA


