Raisi wa zamani wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amepinga kazi inayofanywa na raisi mpya wa klabu hiyo, Joan Laporta baada ya kuruhusu mchezaji bora wa klabu hiyo Lionel Messi kuondoka.

“Wamemuacha Messi aondoke na kwangu hayo ni maamuzi mabaya” Bartomeu alisema akiongea na vyombo vya habari.
“Kucheza bila Messi kumeonyesha mambo mengi yamebadilika.
“Kama raisi, Sikutaka Messi aondoke na nilifanya kila ninaloweza kuhakikisha jambo hilo halotokei.”
Bartomeu pia amesimama na kutetea bodi yake inayoendelea kukosolewa na wadau wengi wa klabu ya Barcelona, kutokana na matatizo ya kiuchumi yanayoikumba klabu hiyo mpaka sasa.
Josep pia alihusika kumteua kocha wa sasa wa klabu hiyo, Ronald Koeman na anaamini mholanzi huyo anastahili na ni mtu sahihi wa kuifundisha timu hiyo.
Fanya wiki yako iwe ya kuvutia zaidi, tunaelekea Los Angeles kutengeneza mkwanja na kasino maridhawa ya LA Rouge kutoka katika kasino za mtandaoni za meridianbettz, Fursa ya kufurahi huku unajaza pochi yako.

CHEZA HAPA

