Ikiwa ni masaa machache yamepita tangu urejeo wa kipenzi cha wanasimba, Clatous Chama, mwenyewe ameibuka na kauli nzito na yenye kutia Imani kwa mashabiki alipozungumza mara ya kwanza baada ya kutambulishwa na wekundu hao wa Msimbazi.
Licha ya Simba kutokuwa na mwanzo mzuri wa msimu, kiungo huyo mshambuliaji mwenye rekodi ya kufunga mabao mengi kwenye mashindano ya kimataifa, amesema bado hakuna sababu ya kukata tamaa amesisitiza kuwa muda upo kwa timu hiyo kuamka na kusonga mbele na kurejea tena kwenye utawala wa soka la Tanzania na Afrika.
Chama amesema matokeo yasiyoridhisha waliyoyapata Simba katika michezo ya awali haipaswi kuwavunja moyo wachezaji, kwani bado msimu una safari ndefu na nafasi ya kurekebisha makosa ipo wazi.
“Matarajio ya msimu hayajatimia kwa matokeo yaliyopatikana kwenye mechi za mwanzo mwa msimu huu, sio mazuri, lakini muda bado upo. Hatujachelewa, tutaamka na kufanya kazi, na mwisho wa msimu tutakuwa na furaha,” amesema Chama.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Ameeleza kuwa kilicho muhimu kwa sasa ni kuongeza nguvu, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wachezaji ili kupambana kwa ajili ya nembo ya Simba na kufanikisha malengo waliyojiwekea.
Chama amesisitiza kuwa ana imani kubwa na kikosi kilichopo, akiamini kuwa kwa bidii, nidhamu na kujituma, Simba itaweza kurejea kwenye mstari na kuonyesha kiwango kinachotarajiwa na mashabiki wake.
Akizungumzia kurejea kwake ndani ya kikosi, Chama amesema anafahamu matarajio makubwa ya mashabiki wa Simba, jambo linalompa motisha ya kuongeza juhudi, nidhamu na kujitoa kwa hali na mali ili kuisaidia timu kufikia malengo ya msimu huu.