Nyota wa kimataifa wa Uswisi, Alisha Lehmann, yuko mbioni kurejea rasmi kwenye Ligi Kuu ya Wanawake England (WSL) baada ya kuonekana akifanya mazoezi na Leicester City siku ya Jumatano. Mshambuliaji huyo, ambaye ndiye mchezaji wa kike anayefuatiliwa zaidi duniani, anajiandaa kuondoka Como ya Italia ili kujiunga na The Foxes katika harakati za kuhakikisha wanabaki kwenye ligi kuu, huku mechi dhidi ya klabu yake ya zamani West Ham United ikitarajiwa kuwa mechi yake ya kwanza mapema Jumapili hii.
Alisha Lehmann tayari ameanza maandalizi ya maisha mapya England baada ya kufika katika kituo cha mazoezi cha Leicester City, Belvoir Drive, na kujiunga na kikosi cha kwanza. Kwa mujibu wa The Athletic, uwepo wake mazoezini unaashiria kuwa dili hilo liko hatua za mwisho, baada ya klabu hiyo ya Midlands Mashariki kufanya kazi kwa karibu wiki mbili kukamilisha usajili wake.
Tetesi kuhusu mustakabali wa Alisha Lehmann ziliongezeka mwishoni mwa wiki iliyopita alipokosekana kwenye kikosi cha Como kilichocheza dhidi ya Napoli. Sasa imebainika kuwa mshambuliaji huyo yuko kwenye mazungumzo ya kurejea WSL, akikatisha safari yake ya Italia.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa sasa Leicester City wanashika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa ligi, wakiwa na tofauti ya pointi tano dhidi ya Liverpool walioko mkiani. Uongozi wa klabu unaonekana kuwa na dhamira ya wazi ya kujihakikishia usalama mapema na kuepuka presha ya kupambana na janga la kushuka daraja.
Alisha Lehmann anaungana na wachezaji wengine wenye uzoefu waliotua klabuni hapo mwezi huu, akiwemo beki Ashleigh Neville kutoka Tottenham, mshambuliaji Rachel Williams kutoka Manchester United na Sarah Mayling aliyejiunga kwa mkopo kutoka Aston Villa.